Onyo La Maangamizi Yanayokuja
2Bwana asema,
“Nitafagia kila kitu
kutoka kwenye uso wa dunia.”
3“Nitafagilia mbali watu na wanyama;
nitafagilia mbali ndege wa angani
na samaki wa baharini.
Wafanyao maovu watapata tu kokoto,
nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,”
asema Bwana.


